Wanawake Watumishi wa wamchao wampendao Kristo

Idara ya Wanawake imeanzishwa kwa mujibu wa ibara ya 20 sehemu ya 7 ya katiba ya Tanzania Assemblies of God. Hivyo kutokana na msingi huo Idara ya WWK imeandaa taratibu na muongozo wa Idara ya WWK kwa msingi wa kuongoza na kusimamia shughuli zote za Idara hii.

Dhima Yetu

Kuwa na wanawake wa kanisa la TAG mbao ni jeshi halisi la Bwana Yesu, walio jaa nguvu za roho mtakatifu, wenye kasi yakueneza na kutegemeza injili ambao maisha yao na ya jamii inayowazunguka huwa bora kwa mjibu wa kanuni za kibiblia. Pia idara ya WWK ipo kwaajili ya kuwaunganisha wanawake wote wa kanisa la TAG kitaifa na kanisa la mahali pamoja kwa kuwakuza kiroho, kuwapandikiza maono na mzigo wa kutumika na kutoa mafundisho yatakayowawezesha wanawake katika kanisa ili kutimiza agizo kuu kwa kutenda na kutoa mali zao

Maadili yetu

  1. Uaminifu kwa Biblia kwa kuishi mafundisho yake.
  2. Kuwajibika kijamii tukidhihirisha upendo na Haki ya Mungu katika maneno na matendo.
  3. Kufanya pamoja kama timu kwa kua na mahusiaono mema baina yetu na watu wengine.
  4. Kuvuna Kimkakati.
  5. Kuwawezesha viongozi.
  6. Kukua kimkakati.
  7. Utawala wa fedha unaowajibika.

Makusudi yetu

  1. Kuiletea Nyumba baraka kwa kua mke bora katika familia
  2. Kuliletea kanisa baraka kwa kushiriki huduma zote zinazohusu kanisa la mahali pamoja na kutoa fungu la kumi na michango yote ya kanisa kwa Uaminifu.
  3. Kumletea mchungaji na familia yake baraka kwa kumuombea mchungaji na familia yake pamoja na kuwasaidia katika mahitaji mengine.
  4. Kukiletea kijiji/mtaa baraka kwa kushiriki huduma zute za kijamii na kuonesha upendo wa kweli kimaneno na matendo.

Sisi ni Nani nani?

Wanawake wanaotangaza Injili ni jeshi kubwa

Idara ya WWK ni moja kati ya idara za kanisa la Tanzania Assemblies of God inayohusika na kupanga na kusimamia shughuli za kimkakati za wanawake katika ngazi zote za kanisa. soma zaidi

Kuhusu Uongozi

Mnamo mwaka 2008, Mchungaji Dr. Barnabas Mtokambali alichaguliwa kuwa askofu mkuu wa awamu ya tatu ya kanisa la Tanzania Assemblies of God. Ndipo Mrs. Faraja Hamuli akateuliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa WWK. Pamoja naye, ilikuwepo kamati ya utendaji ambayo wajumbe wake walikuwa ni Mrs. Eshimendi Swai (Makamu mkurugenzi Mkuu), Mrs. Josephine Manda (Katibu Mkuu), Mrs. Neema seng'enge (Mtunza hazina Mkuu) na Mrs. Gladmary Mtokambali (mshauri Mkuu).

kamati kuu ya Idara kitaifa

Wanawake watumishi wa Kristo.

Hii ndio kamati kuu tendaji kitaifa katika idara ya WWK.

Habari za Hivi Karibuni

Matukio ya Hivi karibuni kwa mwezi huu

Mei

Tanzia

Familia ya makao makuu ya TAG inachukua wakati huu kutoa taarifa ya msiba wa aliyekua Mkurugenzi Kuu wa Idara ya Elimu Kitaifa Rev. Jonas Mkoba uliotokea Tarehe 01 mei 2023.

5 - 11 Jun

Wiki ya Idara ya Watoto na Wanafunzi kitaifa

Idara ya watoto na wanafunzi kitaifa inachukua nafasi hii kuwatangazia waliimu na viongozi wa Idara ya watoto wote wa kanisa la TAG kua wiki la Idara litaanza hivi karibuni. Hivyo basi watoto na wanafunzi wote wanasisitizwa kuhudhuria katika ratiba zote sawa sawa na walivyopangiana katika kanisa la mahali pamoja.

12 - 16 Jun

Mkutano Mkuu wa CA's

Kutakua na Mkutano Mkuu wa Vijana yaani CA's ambao utafanyika CBC Dodoma hivyo Vijana wote mnahimizwa kuhudhuria bila kukosa.