TAMKO KUHUSU USHOGA
Kanisa la TAG limetoa Rasmi Tamko kuhusu Ushoga. Ili kupata nakala ya tamko hili.Bofya Hapa

Mfuko wa Mafao wa Tumaini (TPF) ulianzishwa 01/01/2019 na kanisa la TAG ili kutoa huduma za hifadhi ya jamii kwa watumushi wake.
Kuwa Mfuko wa mafao wa mfano kwa mifuko mingine ya ziada nchini
Uwazi, Uaminifu, Uadilifu, Uwajibikaji, Ubunifu, Kufanya kazi kwa kushirikiana na Huduma kwa wakati
Kutoa huduma bora ya hifadhi ya jamii kwa watumishi kwa kuzingatia misingi ya imani ya kanisa
Kusudi la msingi la pensheni ya uzee ni kumhakikishia usalama wa kipato mtumishi aliyeishiwa nguvu kwa sababu ya uzee. Mtumishi anapokea kipato kila mwezi.
Pensheni ya urithi inalipwa kwa wategemezi wa mtumishi mwanachama wa TPF aliyepoteza uhai. Mafao ya urithi yamekusudiwa kufidia upotevu wa msaada wa kiuchumi uliokuwa ukitolewa na mtumishi aliyepoteza uhai.
Pensheni ya ulemavu inalipwa kwa mtumishi aliyepoteza uwezo wa kufanya kazi kwa sababu ya ulemavu wa kudumu uliosababishwa na ajali au ugonjwa
Mfuko wa Mafao wa Tumaini (TPF) upo kwa ajili ya kukuhudumia wewe Mchungaji wa kanisa la Tanzania Assemblies of God
Kanisa la TAG limetoa Rasmi Tamko kuhusu Ushoga. Ili kupata nakala ya tamko hili.Bofya Hapa
Familia ya makao makuu ya TAG inachukua wakati huu kutoa taarifa ya msiba wa aliyekua Mkurugenzi Kuu wa Idara ya Elimu Kitaifa Rev. Jonas Mkoba uliotokea Tarehe 01 mei 2023.
Idara ya watoto na wanafunzi kitaifa inachukua nafasi hii kuwatangazia waliimu na viongozi wa Idara ya watoto wote wa kanisa la TAG kua wiki la Idara litaanza hivi karibuni. Hivyo basi watoto na wanafunzi wote wanasisitizwa kuhudhuria katika ratiba zote sawa sawa na walivyopangiana katika kanisa la mahali pamoja.
Kutakua na Mkutano Mkuu wa Vijana yaani CA's ambao utafanyika CBC Dodoma hivyo Vijana wote mnahimizwa kuhudhuria bila kukosa.