Miaka kumi na tatu ya Moto wa uamsho tunamtaka Bwana na nguvu zake






Kuhusu Idara ya Uinjilisti
Huduma ya Uinjilisti ilianza rasmi Mwaka 1940 kupitia Wazee wetu (Wainjilisti watano); Rev Emmanuel Lazaro, Rev Moses Kulola, Rev Christian Kiwia, Ev Mathias Ng’andu na Rev Daudi Kuselya. Hawa walikuwa Wainjilisti wa mwanzoni kabisa ambao walihubiri kila kona ya Tanzania na kuhakikisha wanapanda makanisa ...Mwaka 2004, Idara ya Uinjilisti ilianzishwa rasmi katika kanisa la TAG, baada ya pendekezo la kuanzishwa kwake na kupitishwa na Halmashauri Kuu. Pamoja na mikutano Mikubwa ya Injili iliyofanyika huko nyuma, bado hapakuwa na chombo rasmi kitaifa cha kuratibu huduma hizi za Uinjilisti isipokuwa kulikuwa na Kamati tu zilizoundwa kwa kusudi husika la kuandaa mikutano hiyo mpaka mwaka 2004 ambapo Idara ya Uinjilisti Kitaifa ilipoanzishwa rasmi.
Bofya hapa kutembelea tovuti yetu

layout styles

DHIMA

Ni kuhakikisha Injili inahubiriwa kwa nguvu za Roho Mtakatifu, Kwa njia inayoendana na mazingira ili watu wa Tanzania na ulimwenguni kote wapate kusikia habari za Bwana na Mwokozi Yesu Kristo kwa lengo la kuwafanya wawe Wanafunzi wake.

KUSUDI

  • Kuhamasisha na kueneza huduma za Uinjilisti kitaifa.
  • Kuleta Uamsho na kutunza utakatifu ili moto wa Uamsho usizimike.
  • Kuibua na kuibua vipawa vya uinjilisti wa ngazi mbalimbali.

MAADILI

  • Uaminifu kwa Biblia.
  • Uadilifu.
  • Wajibu kwa jamii kwa kuonesha taswira ya upendo na haki kwa watu wote.
  • Kuvuna kwa pamoja.
  • Kuvuna Kimkakati.

VIONGOZI WA IDARA KITAIFA

Habari za Hivi Karibuni

Matukio ya Hivi karibuni kwa mwezi huu

Mei

Tanzia

Familia ya makao makuu ya TAG inachukua wakati huu kutoa taarifa ya msiba wa aliyekua Mkurugenzi Kuu wa Idara ya Elimu Kitaifa Rev. Jonas Mkoba uliotokea Tarehe 01 mei 2023.

5 - 11 Jun

Wiki ya Idara ya Watoto na Wanafunzi kitaifa

Idara ya watoto na wanafunzi kitaifa inachukua nafasi hii kuwatangazia waliimu na viongozi wa Idara ya watoto wote wa kanisa la TAG kua wiki la Idara litaanza hivi karibuni. Hivyo basi watoto na wanafunzi wote wanasisitizwa kuhudhuria katika ratiba zote sawa sawa na walivyopangiana katika kanisa la mahali pamoja.

12 - 16 Jun

Mkutano Mkuu wa CA's

Kutakua na Mkutano Mkuu wa Vijana yaani CA's ambao utafanyika CBC Dodoma hivyo Vijana wote mnahimizwa kuhudhuria bila kukosa.