TAMKO KUHUSU USHOGA
Kanisa la TAG limetoa Rasmi Tamko kuhusu Ushoga. Ili kupata nakala ya tamko hili.Bofya Hapa

Miaka kumi na tatu ya moto wa Uamsho tunamtaka Bwana na Nguvu zake.
Kanisa la Tanzania Asssemblies of God lilipoanza mwaka 1939 halikua na chuo chochote cha Biblia wala mafunzo yeyote rasmi yaliyotumika kuandaa Watumishi. wamishenali walihubiri Injili na watu waliokoka na miongoni mwa watu waliookoka waliosikia wito wa Uwalithibitishwa na viongozi na kuingia shambani na kumvunia Bwana mavuno. Baadaye ikaonekana kuna uhitaji wa mafunzo rasmi ya kuwaandaa Watumishi kwa ajili ya kulifikia taifa kwa Injili ya Bwana Yesu Kristo. Ndipo mnamo mwaka 1980 kamati kuu ya wakati huo chini ya Uongozi wa Mchungaji Emmanueli Lazaro (Askofu Mkuu), Mchungaji Enos Kameta (Makamu Askofu Mkuu) na Mchungaji Solomoni Mwagisa (katibu Mkuu) walikaa na kushauriana na WWamishenari waliokuwepo wakati huo na kwa pamoja walikubaliana kuwepo kwa Idara ya Elimu na huo ndio ukawa mwanzo wa Idara hii. Bofya hapa kutembelea tovuti yetu
Kua na viongozi watumishi waliojitoa kwa Mungu na neno lake, waliobadilishwa kiroho na kuongozwa na Roho mtakatifu, Ili kuyafikia na kuyagusa mataifa kimkakati na injili ya Yesu Kristo.
Kuandaa, kuwezesha na kukuza viongozi watumishi wenye elimu bora ya kipentekoste, ustadi, uadilifu na shauku ya kulizidisha kanisa na kuufikia ulimwengu na injili kwa nguvu za Roho mtakatifu.
|
Kanisa la TAG limetoa Rasmi Tamko kuhusu Ushoga. Ili kupata nakala ya tamko hili.Bofya Hapa
Familia ya makao makuu ya TAG inachukua wakati huu kutoa taarifa ya msiba wa aliyekua Mkurugenzi Kuu wa Idara ya Elimu Kitaifa Rev. Jonas Mkoba uliotokea Tarehe 01 mei 2023.
Idara ya watoto na wanafunzi kitaifa inachukua nafasi hii kuwatangazia waliimu na viongozi wa Idara ya watoto wote wa kanisa la TAG kua wiki la Idara litaanza hivi karibuni. Hivyo basi watoto na wanafunzi wote wanasisitizwa kuhudhuria katika ratiba zote sawa sawa na walivyopangiana katika kanisa la mahali pamoja.
Kutakua na Mkutano Mkuu wa Vijana yaani CA's ambao utafanyika CBC Dodoma hivyo Vijana wote mnahimizwa kuhudhuria bila kukosa.