TAMKO KUHUSU USHOGA
Kanisa la TAG limetoa Rasmi Tamko kuhusu Ushoga. Ili kupata nakala ya tamko hili.Bofya Hapa

Miaka kumi na tatu ya Moto wa uamsho tunamtaka Bwana na nguvu zake
Idara ya Watoto na Wanafunzi ni Idara ndani ya kanisa la TAG, lilianzishwa rasmi Mwaka 1994 kufuatia mkutano wa viongozi wa Kanisa la Assemblies of God, barani Afrika, “Africa Assemblies of God Alliance” (AAGA) uliofanyika Nairobi, nchini Kenya mwaka mwaka 1993. Idara hii ilianzishwa ikiwa ni utekelezaji wa maazimio muhimu katika mkutano huo wa (AAGA). Mwaka huo wa 1994 kanisa la TAG lilikuwa linaongozwa na Askofu Mkuu Rev. Ranwell Mwenisongole na alimteua marehemu Mchungaji Joseph Justine kuwa Mkurugenzi Mkuu. Kadhalika, marehemu Mchungaji Jeremiah Kimaro aliteuliwa kuwa Makamu Mkurugenzi Mkuu na Mch. Everhard Mloka kuwa Katibu Mkuu. Huo ndio ukawa mwanzo mzuri wa Idara hii.
Bofya hapa kutembelea tovuti yetuKuwafanya watoto wa Tanzania kuwa wanafunzi wa Yesu Kristo, waliojazwa Roho Mtakatifu na kuukulia Wokovu, hatimaye wawe watumishi bora wa Bwana Yesu Kristo katika Kanisa lake.
Idara ya watoto ipo ili Kumhubiri Kristokwa watoto wa Tanzania, mashuleni, mitaani, majumbani, Kanisani na kuwafanya wanafunzi wa Yesu Kristo.
Kanisa la TAG limetoa Rasmi Tamko kuhusu Ushoga. Ili kupata nakala ya tamko hili.Bofya Hapa
Familia ya makao makuu ya TAG inachukua wakati huu kutoa taarifa ya msiba wa aliyekua Mkurugenzi Kuu wa Idara ya Elimu Kitaifa Rev. Jonas Mkoba uliotokea Tarehe 01 mei 2023.
Idara ya watoto na wanafunzi kitaifa inachukua nafasi hii kuwatangazia waliimu na viongozi wa Idara ya watoto wote wa kanisa la TAG kua wiki la Idara litaanza hivi karibuni. Hivyo basi watoto na wanafunzi wote wanasisitizwa kuhudhuria katika ratiba zote sawa sawa na walivyopangiana katika kanisa la mahali pamoja.
Kutakua na Mkutano Mkuu wa Vijana yaani CA's ambao utafanyika CBC Dodoma hivyo Vijana wote mnahimizwa kuhudhuria bila kukosa.