TAMKO KUHUSU USHOGA
Kanisa la TAG limetoa Rasmi Tamko kuhusu Ushoga. Ili kupata nakala ya tamko hili.Bofya Hapa

Miaka kumi na tatu ya Moto wa uamsho tunamtaka Bwana na nguvu zake
CASFETA ni jumuiya ya wanafunzi walio mabalozi wa Kristo Tanzania yenye malengo tangu kuanzishwa kwake. Ushirika huu ni hitaji la wanafunzi walioko shule za sekondari na vyuoni kumuabudu Mungu kulingana na imani ya Kipentekoste. CASFETA ilianzishwa mwaka 1992. Wazo lake lilianzia kwa viongozi wa Idara ya vijana wa TAG, yaani Christ’s Ambassadors (CAs). Aliyekuwa Katibu Mkuu wa CAs, mchungaji Uswege Mwakisyala alikuwa ndiye Mwenyekiti wa kamati ya watu watatu. Askofu Mkuu wa wakati huo Mchungaji Ranwel Mwenisongole alijibu kwa barua yake ya tarehe 8/10/1992, kuikubali huduma hiyo ianzishwe na kusimamiwa na idara ya Vijana CAs. CASFETA ilipata Mkurugenzi mpya 2008, Mch. Dkt. Huruma Nkone ambaye katika uongozi wake iliendelea kukua na kuzifikia shule, vyuo na vyuo vikuu vingi hapa nchini Tanzania, ambapo hadi kufikia mwaka 2020 kumekuwa na matawi zaidi ya elfu mbili mia tisa (2,900) nchini kote. Bofya hapa kutembelea tovuti yetu
Kuwa kizazi kinachotembea katika nguvu za Roho Mtakatifu na kuubadilisha ulimwengu kwa Neno la Mungu.
Kuwafikia wanafunzi wote kwa Injili ya Kristo kimkakati na kuwajenga kiroho kwa njia ya Kuabudu, Ushirika, Kufuasa ili waweze kuwahudumia watu wote kwa uwezo wa Roho Mtakatifu.
Kuwafundisha wanafunzi kuyaishi maadili ya kikristo, kupiga vita matendo yote yanayoharibu jamii kama vile; Magonjwa ya zinaa, UKIMWI, Utoaji mimba, Ulevi, Utumiaji madawa ya kulevya, Ushoga, Usagaji, Ubakaji, pamoja na matendo mengine yote maovu.
Kanisa la TAG limetoa Rasmi Tamko kuhusu Ushoga. Ili kupata nakala ya tamko hili.Bofya Hapa
Familia ya makao makuu ya TAG inachukua wakati huu kutoa taarifa ya msiba wa aliyekua Mkurugenzi Kuu wa Idara ya Elimu Kitaifa Rev. Jonas Mkoba uliotokea Tarehe 01 mei 2023.
Idara ya watoto na wanafunzi kitaifa inachukua nafasi hii kuwatangazia waliimu na viongozi wa Idara ya watoto wote wa kanisa la TAG kua wiki la Idara litaanza hivi karibuni. Hivyo basi watoto na wanafunzi wote wanasisitizwa kuhudhuria katika ratiba zote sawa sawa na walivyopangiana katika kanisa la mahali pamoja.
Kutakua na Mkutano Mkuu wa Vijana yaani CA's ambao utafanyika CBC Dodoma hivyo Vijana wote mnahimizwa kuhudhuria bila kukosa.