Miaka kumi na tatu ya Moto wa uamshotunamtaka Bwana na nguvu zake
Ijue Idara ya Vijana
Jina la Idara ni Tanzania Assemblies of God - Christ's Ambassadors (CA's); Yaani ikiwa na maana ya Vijana mabalozi wa Kristo.'Kimsingi ni Idara ya Vijana'.
MAONO
Maono ya Idara ya Vijana ni kua na Vijana:-
Walio jaa Roho mtakatifu kikamilifu.
Walio hamasika kihuduma.
Wenye mzigo na uwezo wa kuvuna roho zilizopotea kwa ufanisi mkubwa.
Kua na viongozi waaminifu na wawajibikaji katika ngazi zote.
DHIMA
idara ya Vijana wajumbe wa Kristo kwaajili ya: -
Kuhamasisha vijana.
Kuunganisha Vijana.
Kulea vijana katika malezi bora.
Kupandikiza vijana Mzigo na Maono ya; -
Kuabudu kwa hiari yao baada ya kufundishwa umuhimu wa kumuabudu MUNGU.
Kutumika kwa bidii na viwango vya juu.
Kushirikiana wao kwa wao na kanisa lao.
Kujifunza neno la MUNGU na kuliishi maishani mwao.
Kua viongozi bora na wenye utayari wa kujitoa kwa gharama yeyote.
MAKUSUDI
Makusudi ya Idara ni:-
Kushuhudia.
Idara inawaandaa vijana kwa mafunzo mbalimbali na kuwahamasisha ili kwa kutumia mbinu na njia mbalimbali waweze kufanya uinjilisti wenye Nguvu utawawezesha kuwaleta watu wenyedhambi kwa Yesu.